Ulimwengu umeingia katika mfumo wa teknolojia iliyokuwa ,hivyo kupelekea kuachana na mfumo wa analojia na kwenda na dijital hii ina rahisisha namana nzuri ya mawasiliano,pamoja na upatikanaji wa taarifa mbalimabali ndani na nje ya nchi,pia ni mabadiliko ambayo yanaendana sambamba na ubunifu wa kidijital
Ujuzi wa kidigitali ni uwezo wa kutumia mbinu mpya za kiteknolojia katika kutatua matatizo ya kiutendaji katika nafasi za uandishi wa habari na kupata matokeo chanya yanayomfanya kutambulika katika ulimwengu wa digitali.
Asha D. Abinallah ambaye ni kiongozi wa kampuni ya Tech & Media Convergency inayotoa mafunzo kwa waandishi wa habari wanawake kuhusu uandishi wa kidigitali ikiwa na lengo la kuwaendeleza waandishi wa habari katika uandishi wa habari kutumia teknolojia iliyokuwa.
Amesema kupitia program hiyo maalumu ya mafunzo ya ujuzi kidigitali inawapa waandishi kupata uelewa na ujuzi wa namna ya kuandaa na kutengeneza maudhui kwa ajili ya kuyatumia katika majukwaa ya kidijitali.
Abinallah ameongeza kuwa kutumia mitandao hiyo kama majukwaa ya uandishi wa habari kwa kuandaa vipindi, habari, makala wanavyoandaa inasaidia kutengeneza fursa za kujiongezea kipato.
Lilian Urio ni mwandishi wa kidigitali ambaye pia ni mkufunzi wa mafunzo ya uandishi wa kiditali, amesema mwandishi wa habari anapaswa kujua stadi za kiditali ambazo ndio mwongozo katika kuandaa maudhui pamoja na kujua namna ya kutumia majukwaa ya digitali.
“Ili kuweza kupata habari na data kwa usahihi, ili kuandaa maudhui bora na inayoeleweka kwa jamii ni lazima mwandishi ukubali kubadilika na uendane na kasi ya kukumbatia huu ujuzi wa kidijitali.” amesema Lilian Urio.
Naye Peter Helatano mwandishi wa habari anaye wakilisha Global tv online Mkoani Rukwa ,amesema ifike mahali waandishi wa habari waone umuhimu wa kukumbatia ujuzu huu wa dijitali kwa kuwa kunafursa nyingi kwa mwanahabari ambazo zitawaongezea ujuzi,,amesema kupitia simu janja anayotumia inaweza kufanya vitu vingi sana amesema ndio ofisi yake anayotumia kupata habari,na kutuma habari anazoandaa.
Hata hivyo mwandishi wa habari wa kidigital ni vyema akazingatia kazi za kidijitali ambazo zitamsaidia kuandaa maudhui ikiwa ni pamoja na kujua nanma nzuri ya kutumia mitandao ya kijamii kukusanya data pamoja na kupata uhakika wa kuandaa maudhui bora kwa kutumia umakini mzuri.
Kupitia uandishi wa habari wa kidigitali kuna faida mbalimbali mwandishi anaweza kuzipata ikiwa ni pamoja na kujiongezea kipato na kuongeza mawazo mapya ya habari kupitia waandishi wengine,na kuongeza ujuzi katika kazi yako ya uandishi wa habari ikiwa nipamoja na kujifunza namna watu wanavyo andika habari au kutangaza habari.
ANNA MALISA | NDINGALA FM
DIGITAL JOURNALISTS 2021/22
BORESHA HABARI PROJECT
ANNA MALISA
DIGITAL JOURNALIST 2021/22
BORESHA HABARI PROJECT